Wagonjwa majeruhi wa vita 16 wahamishwa kutoka hospitali ya Kamal Adwan kuwapeleka katika hospitali ya Al-Shifa
MP3•Trang chủ episode
Manage episode 445184308 series 2027789
Nội dung được cung cấp bởi UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations. Tất cả nội dung podcast bao gồm các tập, đồ họa và mô tả podcast đều được UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations hoặc đối tác nền tảng podcast của họ tải lên và cung cấp trực tiếp. Nếu bạn cho rằng ai đó đang sử dụng tác phẩm có bản quyền của bạn mà không có sự cho phép của bạn, bạn có thể làm theo quy trình được nêu ở đây https://vi.player.fm/legal.
Operesheni ya vikosi vya jeshi la Israel inayoendeea Kaskazini mwa Gaza kwa njia ya anga na ardhini kukabiliana na wapiganaji wa kundi la wanamgambo wa Kipalestina la Hamas yamelifanya eneo hilo kukatwa na sehemu zingine za Gaza, kwa kiasi kikubwa raia wakikosa huduma za msingi kama chakula, elimu na matibabu. Hospitali karibu zote Gaza Kaskazini hazifanyi kazi na iliyosalia ni Kamal Adwan nayo ikitoa huduma kwa kiasi kidogo sana kutokana na ukosefu wa vifaa, wahudumu wa afya na mafuta. Majeruhi wa vita wamezidi uwezo wa hospitali hiyo ndio maana ikaamua kuomba msaada kutoka shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO kuhamisha majeruhi hao kwenda hospitali Al-Shifa mjini Gaza. Katika makala hii Flora Nducha anamulika zoezi hilo la kuhamisha majeruhi.
…
continue reading
100 tập